Saturday, 9 July 2016

MUSA SAID AREJEA KUTOKA KATIKA KAMBI YA KIMATAIFA YA COPA COCA- COLA, UFARANSA



Nyota wa soka aliyefanya vizuri michezo ya Shule za Sekondari (UMISETTA) Mussa Bakari akiwasili ndani ya uwanja cha ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kutokea katika kambi ya Kimataifa ya Copa Coca-Cola iliyofanyika jijini Paris nchini Ufaransa. 
Meneja Msaidizi wa Chapa ya Coca – Cola, Mariam Sezinga (kushoto) akimpokea kwa shangwe nyota wa soka aliyefanya vizuri michezo ya Shule za Sekondari (UMISETTA) Mussa Bakari (katikati) mara baada ya kuwasili ndani ya uwanja cha ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kutokea katika kambi ya Kimataifa ya Copa Coca-Cola iliyofanyika jijini Paris nchini Ufaransa. Pembeni ni Pamela Lugenge (kulia) mmoja wa Afisa Masoko. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog. 
Meneja Msaidizi wa Chapa ya Coca – Cola, Mariam Sezinga (kushoto) akimkabidhi taji la maua nyota wa soka aliyefanya vizuri michezo ya Shule za Sekondari (UMISETTA) Mussa Bakari mara baada ya kuwasili ndani ya uwanja cha ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kutokea katika kambi ya Kimataifa ya Copa Coca-Cola iliyofanyika jijini Paris nchini Ufaransa. Pembeni ni Pamela Lugenge (kulia) mmoja wa Afisa Masoko. 
 Meneja Msaidizi wa Chapa ya Coca – Cola, Mariam Sezinga (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na nyota wa soka aliyefanya vizuri michezo ya Shule za Sekondari (UMISETTA) Mussa Bakari (katikati) pamoja na Pamela Lugenge (kulia) mmoja wa Afisa Masoko.

DOLE LA KATI LA MBUNGE MR SUGU LILILOSABABISHA AFUNGIWE BUNGENI



Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi 'Mr Sugu' akiwaonesha wabunge wa CCM dole la kati Bungeni Dodoma hivi karibuni, kitendo ambacho kilitafsiliwa na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuwa ni tusi, hivyo kupewa adhabu ya kutohudhuria vikao kumi vya Bunge. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)

Tuesday, 5 July 2016

MULTICHOICE TANZANIA KUBADILI MAISHA YA WATOTO YATIMA

Zikiwa zimesalia siku kadhaa kabla ya kusherekea sikukuu ya Eid El Fitri, Kampuni ya Multichoice Tanzania ambao ndiyo wasambazaji wa ving’amuzi vya DSTV nchini imetoa msaada wa vitu mbalimbali kwa watoto yatima ambao wanaishi katika kituo cha Al-Madina kilichopo Tandale kwa Tumbo, misaada ambayo kwa namna moja au nyingine inaweza kusaidia kubadilisha maisha ya watoto hao.
 
Misaada ambayo imetolewa kwa watoto hao ni Cherehani 4, kapeti 12, vikombe 60, sahani 40, magodoro 11, shuka 40, tenga za nguo 3, jagi 6, beseni kubwa 3, sufuria 9, chupa za chai 4 na mikeka 6.
 
Akizungumzia misaada hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande alisema msaada huo ni mwendelezo wa misaada ambayo Multichoice imekuwa ikitoa kwa kituo hicho kwa lengo la kuwasaidia kuishi maisha bora lakini pia kuwapatia msaada ambao unaweza kuwasaidia kuwa na uwezo wa kuingiza kipato.
Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande akizungumza kuhusu msaada ambao wameutoa kwa kituo cha Al–Madina.
 
“Multichoice tumekuwa tukitoa misaada yetu kwa kituo hiki tangu 2009 na leo tumewaletea mwingine ikiwa ni kila mwaka tunafanya hivyi lakini kwa mwaka huu tumeleta pia Cherehani ambazo zitawasaidia kupata kipato,
 
“Pamoja na hayo pia tumewafungia king’amuzi ambacho watoto watakuwa wakiangalia vipindi balimbali baada ya kurejea nyumbani na tuna chaneli mbalimbali za vipindi vya watoto na burudani kwahiyo tunaamini kuwa watoto watafurahi,” alisema Chande.
 
Nae mlezi wa kituo hicho, Bi. Kuruthum Yusuf aliwataja Multichoice kama kampuni ambayo imekuwa mstari wa mbele kuwapatia misaada na kuyaomba makampuni mengine kuwa na utaratibu kama wa Multichoice wa kuwasaidia misaada kutokana na kuwa na idadi kubwa ya watoto ambao wanahitaji misaada ili kuboresha maisha yao.
Mlezi wa kituo cha watoto yatima cha Al-Madina akizungumza kuhusu msaada ambao wamepokea na jinsi ambavyo Multichoice Tanzania imekuwa ikiwapatia misaada. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Mharage Chande.
 
“Tangu walipotufahamu wamekuwa wakitupatia misaada kila mwaka, niwashukuru sana kwa moyo wao na kutoa sio utajiri ila tu wana moyo wa kutoa na hata wenngine wanatakiwa kuwa na moyo kama wao (Multichoice) wa kusaidia,” alisema Bi. Kuruthum.
Pamoja na hayo pia, Bi. Kuruthum alieleza kuwa kwa sasa bado wanakabiliwa na changamoto ya vifaa vya shuleni kwa watoto ambao wanasoma.
Kutokana na msaada ambao umetolewa na Multichoice kwa watoto wa kituo cha Al-Madina ambacho kina watoto 57, wasichana wakiwa ni 23 na wavulana ni 34 basi ni wazi kuwa kama wakitumia msaada huo vyema basi kwa namna moja au nyingine wanaweza kubadilisha maisha yao kwa hatua fulani ambayo awali hawakuwa nayo kama vile kutumia cherehani kwa kushona nguo na kujiongezea kipato.
Meneja Uhusiano na Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Sumalu akitoa neno la ufunguzi kuhusu misaada ambayo imekuwa ikitolewa na Multichoice Tanzania pamoja na historia fupi ya kituo hicho.
Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Mharage Chande akimkabidhi Cherehani, mlezi wa kituo cha Al-Madina, Kuruthum Yusuf. Wa tatu kushoto ni Meneja Uhusiano na Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu wakiwa na wafanyakazi wengine wa Multichoice Tanzania.
Meneja Uhusiano na Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu akimpongeza mlezi wa kituo cha Al-Madina, Kuruthum Yusuf baada ya kukabidhiwa misaada na Multichoice Tanzania.

MAMA SAMIA AWATAKA WATANZANIA KUITUNZA AMANI






Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir akitoa Nasaha katika futari Maalum iliyoandaliwa na Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ambapo mufti mkuu aliwataka waislam kutojihusisha na matendo ya Kigaidi kwani hayaendani na maelekezo na mafundisho ya Allah.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitoa neno la shukrani kwa wageni waliojumuika kwenye futari aliyoiandaa nyumbani Oysterbay jijini Dar es Salaam kwake ambapo aliwataka Watanzania kudumisha mani na kuishi kwa upendo

Waalikwa kwenye Futari ilyoandaliwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan wakiswali muda mfupi kabla ya kufuturu.

Sehemu ya Wageni waliohudhuria

Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Kamati ya amani Sheikh Alhad Mussa akizungumza na waalikwa kwenye futari iliyoandaliwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Padri John Solomon akitoa salaam za Kamati ya Amani wakati wa futari iliyoandaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan

SHIRIKA LA MADINI LA TAIFA (STAMIKO) LAANZISHA VITUO SITA VYA KUTOA ELIMU KWA WACHIMBAJI WADOGO MIKOA SITA .




Mkurugenzi wa Shirika la Madini la Taifa Stamiko Deusdedith Magala,akizugumzana na waandishi wa habari hawapo pichani juu ya wameanzisha vituo sita vya kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo katika mikoa sita,leo jijini Dr es Salaam.


Wanyakazi wa Shirika la Madini la Taifa Stamiko wakionesha jinsi walivyoimarisha usalama na uokoaji migodi,leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii)

Akizungumza katika maonyesho ya 40 ya biashara ya Kimataifa Dar es Salaam yanayofanyika katika viwanja vya sabasaba wakati wakionesha jinsi namnausalama na uokoaji unavyofanyika katika mgodi wa Biharamulo, Kaimu Mkurugenzi wa Stamiko Deusdedith Magala, alisema kuwa vituo hivyo vitakuwa katika mikoa sita kwa ajili ya kutoa mafunzo ya usalama kwa wachimbaji wadogo.

Alivitaja vituo hivyo kuwa ni Mkoa wa Kagera, Mara, Mbeya Singida Mwanza na Geita ambavyo watakuwa wanatoa elimu ya usalama kwa wachimbaji wadogo kuepuka ajali migodini.

Hata hivyo aliwataka wachimbaji wadogo kuhakikisha wanafika katika vituo vya stamiko vilivyopo karibu kupatiwa elimu jinsi ya kuepuka ajali zinazotokea migodini mara kwa mara. "Suala la usalama na uokoaji katika Migodi inatakiwa kupewa kipaumbile ili kuepuka ajali za mara kwa mara kwa wachimbaji wadogo wakielimika ajali za migodini zitaepukika,"alisema Magala.

Kwa Upande wake Mjiolojia Mkuu wa Mgodi wa Biharamulo Ayoubb Nyenzi aliyemwakilisha meneja wa mgodi wa dhahabu wa Biharamulo, Amesema Tanzania ina wataalamu wazuri wa kuchimba madini hivyo ni vyema serikali ikawapa nafasi zaidi ili kuhakikisha rasilimali hiyo inaleta manufaa zaidi hapa nchini.

Nyenzi alisema mgodi huo unashirikiana kwa karibu na jamii inayozunguka mgodi ambapo wameweza kutoa madawati 2000 kwa shule pamoja na ujenzi wa shule ya sekondari. Aliendelea kusema wameweza kufanya biashara na wananchi wanaozunguka eneo hilo kwa kuwapatia elimu ya kilimo cha mboga mboga na matunda ambapo wanauzia mgodi na wameweza kujipati milioni 2000.

Naye Mrakibu wa usalama afya na uokoaji Mgodini Fotunatus Japi, alisema suala la usalama lazima lizingatiwe hususani kwa wachimbaji wadogo na wakubwa. Alisema katika mgodi wao wa Biharamulo wamekuwa wakizingatia suala la usalama kwa kuwa iwapo majanga yakitokea kunaathiri soko la dhahabu inayotoa mgodini hapo.

Hata hivyo alisema wanatumia juhudi zote kuhakikisha hakuna majanga na pale yanapotokea kunakuwepo na uokoaji wa uhakika.

MFALME WA AFRO POP TWENTY PERCENT ARUDI KWENYE GEMU KWA KISHINDO NA SAUTI YAKE YA GHARAMA


Na Sultani Kipingo
Mfalme wa Afro Pop nchini Abbas Hamisi Kinzasa almaarufu kama 20% (Twenty per Cent) anavunja ukimya na kurejea kwa kishindo kwenye anga ya muziki,  huku akiwa msanii wa kwanza kusaini mkataba na lebo mpya ya KOMBINENGA inayoendeshwa na producer nguli John Shariza a.k.a Mann Water.
Twenty Percent, ambaye mwaka 2011 alitwaa tuzo saba za Kilimanjaro Music Awards (KTMA) kwa mpigo, huku Mann Water akisomba tuzo mara mbili mfululizo  za producer bora (mwaka 2013 na 2014), tayari amesharekodi vibao vitano na anatarajia kuachia ngoma moja mpya ya kwanza Julai 18, 2016, katika kuandaa albamu yake ya SAUTI YA GHARAMA.
"Nimerudi kuwachinja tena" anasema Twenty Per cent, akiwa anakamilisha kurekodi katika studio za Combination Sounds iliyoko Kinondoni Mkwajuni jijini Dar es salaam. "Nimerudi kurudisha sauti ya gharama  kwa jamii. Sauti inayofundisha. Sauti inayoonya. Sauti inayoburudisha. Sauti inayozengua kila mtu, " anaogeza.
Tayari Tweny Per cent ameshasaini mkataba wa miaka mitano na lebo ya KOMBINENGA, katika hafla fupi iliyofanyika Jumapili katika ofisi za Combination Sounds. Kuanzia sasa shughuli zote za msanii huyu zitasimamiwa na lebo hiyo chini ya Producer Mann Water.
Wakili msomi Iddi M. Gogo wa Alpha Attorneys ndiye aliyefanikisha zoezi hilo la kutiliana saini mkataba lililoshuhudiwa pia na meneja uzalishaji wa Combination Sounds, Rowel Moses.
"Namkubali sana Twenye Pa kwani ni msanii aliyetimia na hutumii shuruba wakati wa kurekodi maana ana kipaji cha ajabu cha kutunga akiwa wima na kukariri hapohapo", anasema Mann Water, ambaye ameshafanya kazi na  wasanii nyota kibao wakiwemo  Lady Jay Dee,  Ali Kiba, Ommy Dimpoz, Christian Bella, MB Dogg, Juma Nature, Mr Blue na wengine wengi.
 Twenty Percent alitamba sana tokea mwaka 2006 kwa wimbo wake wa "Manemane" uliomfanya ashinde tuzo ya KTM, kabla ya kuweka historia ya kusomba tuzo saba kwa mpigo mwaka 2011. wakati huo nyimbo zilizompandisha chati zilikuwa ni "Tamaa Mbaya"  na "Ya nini Malumbano" na "Maisha ya Bongo"   
Mbali na Muziki Twenye Percent pia alitamba sana kwenye tasnia ya filamu ambapo alicheza kwenye mchezo uliofahamika kwa jina lake la 20%. Baada ya hapo akaamua kupumzika kwa muda na kujishugulisha na shughuli za kilimo. "Kilimo kinaendelea vyema na sasa nimeamua kurudi kwenye gemu ili kuwachinja tena" alimalizia, akiinuka kuelekea kwake Kimzichana, Mkuranga, Mkoa wa Pwani, anakoishi.
Producer nguli wa muziki nchini John Shariza a.k.a Mann Water (chini kushoto) akiweka saini kwenye hati ya mkataba wa lebo ya KOMBINENGA kurasimisha usimamizi wa kazi za msanii Abbas Hamisi Kinzasa almaarufu kama 20% (Twenty per Cent) akishuhudiwa na Wakili msomi Iddi M. Gogo wa Alpha Attorneys  (juu kulia) aliyefanikisha zoezi hilo, pamoja na meneja uzalishaji wa Combination Sounds, Rowel Moses (juu kushoto) kwenye studio za Combination Sounds Kinondoni Studio jijini Dar es salaam.

AMOTEL IS THE FIRST LINSENCED MVNO STARTS OPERATIONS IN RURAL TANZANIA




Deputy Minister for Works, Transports & Communications, Hon. Eng. Ngonyani cutting A ribbon to officiate the launch of AMOTEL in Mwanga district. From the left is Board Chairman of AMOTEL, Professor Robert Mabele while on the right is Dr. Eng. Maria Sasabo-the deputy Permanent Secretary for Ministry of Works, Transports & Communications assisting the guest of honour to grace the official launch of AMOTEL as an MVNO with a network code “063” which serves the underserved villages under UCSAF’s projects. 

A cross section of villagers who are the direct beneficiary of AMOTEL’s launch following up the ceremony of AMOTEL’s operations in Mwanga district. The event was graced by the Deputy Minister for Works, Transports & Communications. The direct beneficiary villages are; namely, Ngujini, Songoa and Chanjale villages .

A cross section of villagers who are the direct beneficiary of AMOTEL’s launch following up the ceremony of AMOTEL’s operations in Mwanga district. The event was graced by the Deputy Minister for Works, Transports & Communications. The direct beneficiary villages are; namely, Ngujini, Songoa and Chanjale villages 


The Guest of Honour signing the guests book at the district’s commissioner’s office to officiate the launch of AMOTEL’s rural telephony in Mwanga district. Sitting close to the guest of honour is the Board Chairman of AMOTEL, Prof. Robert Mabele. Others from left is Acting DC Mwanga, next is Eng. Peter Ulanga-CEO , UCSAF. Then, followed by Eng. Brown Japhet, the TTCL-Regional Manager Kilimanjaro. While others from right is Dr. Eng. Maria Sasabo-Deputy Permanent Secretary in the Ministry for Works, Transports & Communications. Then is followed by the TCRA-Northern Zone Office and the last is the Acting DED-Mwanga.

Mr. Philemon Mangu, the AMOTEL’s Chief Technical Officer (CTO) explaining to the guest of honour, Eng. Ngonyani somewhere inside the village of Ngujini-Kisangara Juu in Mwanga district. Standing in the middle is Eng. Peter Ulanga listening attentively to AMOTEL’s CTO. Behind is Retired Judge of the Court of Appeal of Tanzania, Hon. January Msofe who is a widely respected elder of Ngujini village and Mwanga district in general. 

Wednesday, 29 June 2016

MBUNGE WA UKONGA MWITA WAITARA-AFUTURISHA WAPIGA KURA KWAKE

lo1Waziri Mkuu wa zamani na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa,akizungumza katika Futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara(Chadema) kwa wananchi wa jimbo hilo nyumbani kwake Kivule Dar es Salaam juzi.
lo2Waziri Mkuu wa zamani na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa,akizungumza na waandishi wa habari baada aya kushiri Futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara(Chadema),nyumbani kwake Kivule Dar es Salaam juzi.
lo3Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara(Chadema), akizungumza katika Futari aliyowaandalia wananchi wa jimbo hilo nyumbani kwake Kivule Dar es Salaam juzi.
lo4Wananchi wakifuturu Futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara(Chadema),nyumbani kwake Kivule Dar es Salaam juzi.
lo5Wananchi wakifuturu Futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara(Chadema),nyumbani kwake Kivule Dar es Salaam juzi.
lo6Wananchi wakifuturu Futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita Waitara(Chadema),nyumbani kwake Kivule Dar es Salaam juzi.